MASUALA IBUKA
Magonjwa
Aina
- malaria
- mafua
- macho
- ngozi
- meno
- kifua kikuu
- homa ya mapafu
- kifaduro
- zinaa (kaswede/syphilis)
- kipindupindu
- homa ya matumbo
- homa ya mapafu
- shinikizo la damu
- ugonjwa wa moyo
- matumbwitumbwi/machapwi
- saratani
- utapia mlo
- ukambi/surua
- tetewanga
- homa
- malale
Jinsi ya Kujikinga na Magonjwa
- Kula chakula chenye virutubisho vyote na madini
- Kutotumia chumvi, sukari au mafuta mengi
- Kufanya mazoezi
- Kupimwa mara kwa mara
- Kupika vyakula vizuri
- Kunawa mikono na macho
- Kuchemsha maji au kuyatia dawa kabla ya kuyanywa
- Kutozini au kutumia kinga
- Chanjo kwa watoto
- Kutochangia vifaa kama vitana na nyembe na mavazi ili kujikinga na magonjwa ya ngozi.
- Kulala ndani ya neti iliyotiwa dawa
- Kufyeka nyasi karibu na nyumba na kutupa mikebe iliyo na maji
- Kuweka dawa kwenye vidimbwi ili kuua mbu
- Kutotumia vileo kama vile pombe na sigara
- Kuzuia kunyeshewa na mvua na kuvaa mavazi mazito wakati wa baridi au usiku
- Kukohoa au kupiga chafya mtu akiwa ameziba pua na midomo na kutotema kikohozi ovyo
- Kutubu dhambi, kujua Mungu na kuomba kwa afya ya kiroho
Ukimwi
- Ugonjwa unaosababishwa na virusi vya HIV unaofanya mwili kupungukiwa na kinga dhidi magonjwa.
Njia za Maambukizi
- Uzinzi, ubakaji au ulawiti
- Tohara ambapo ngariga anatumia kisu kimoja kwa watahiriwa wote
- Kuchangia vifaa vyenye ncha kali k.v. nyembe, vinyoleo n.k.
- Utumiaji wa sindano moja na vifaa vya upasuati ambavyo havijatiwa dawa au kutokoswa ili kuua viini
- Wanawake kuambukiza watoto wakijifungua
- Kuongezewa damu ambayo haijapimwa au haijapimwa vizuri.
- Utumiaji wa dawa za kulevya kwa kujidunga kwa sindano moja
- Ulevi kumfanya mtu kupotewa na utambuzi kisha kufanya ngono na mtu aliyeambukizwa.
- Kubusu mtu aliye na virusi ukiwa na vidonda kinywani
- Wakati wa ajali watu walio na viini wanapojeruhiwa na kutokwa na damu na inafikia majeraha katika miili ya wasio na hivyo viini
Dalili
- Kukohoa kwa muda mrefu
- Kuendesha kwa muda mrefu
- Kupoteza hamu ya kula
- Kukonda au kupoteza uzani wa zaidi ya kilo 10 kwa muda mfupi
- Mwili kudhoofika/unyonge
- Kunyonyoka nywele
- Jipu lmwilini
- Mwasho mkali katika ngozi
- Vidonda kinywani na kooni
- Homa na kutokwa na jasho jingi usiku
- Magonjwa ya kifua kikuu na homa ya mapafu
- Saratani ya ngozi
- Kuvimba shingoni
- Utaahira wa akili k.v. kusahau na kutokumbuka mambo
Madhara
- Jamaa kuathirika kisaikolojia wakiona mtu wao akiteseka na ugonjwa
- Vifo kwa kuzidiwa na ugonjwa
- Huzuni baada ya mgonjwa kuaga dunia
- Watoto kuachwa wakiwa mayatima baada ya wazazi kufa
- Gharama kubwa ya kugharamia matibabu
- Unyanyapaa/kutengwa/kubaguliwa
- Ndoa kuvunjika kutokana na lawama
- Ubakaji wa watoto wa kike ili kujitakasa
- Kuathiri uchumi wa nchi pesa nyingi zinapotumiwa kununulia dawa za kupunguza makali hata za kifua kikuu
- Serikali kupoteza wataalamu iliyogharamia elimu yao kulazimika kuajiri wataalamu kutoka nje kwa gharama ya juu sana
Jinsi ya Kujikinga
- Kutofanya zinaa kabla na nje ya ndoa
- Walioambukizwa kutumia dawa za kupunguza makali (A.R.Vs)
- Aliyebakwa kupewa dawa za A.R.V kabla ya saa 72
- Kuwapa mama waja mzito wenye virusi dawa kabla ya kujifungua kukinga mtoto
- Ngariba kutotumia kisu kimoja kwa watahiriwa wote
- Kutumia sindano mpya hospitalini na matumizi ya dawa za kulevya
- Kupima damu vizuri kabla ya kuwaongezea wagonjwa
- Kupimwa kabla ya ndoa na mara kwa mara ili kujua hali ili kujikinga dhidi ya maambukizi au kujitunza kama mtu ameambukizwa
- Kutumia mipira
- Walioambukizwa kutofanya mapenzi bila kinga ili wasipate virusi aina tofauti na sugu au magonjwa mengine ya zinaa
- Kula chakula vinavyofaa na kufanya mazoezi
- Kupata matibabu wakati ufaao mtu anapougua magonjwa mengine
- Kumjua Mungu ili kumwamini na kumtumainia ili kuondoa uoga na mahangaiko na hivyo kumwezeha mtu kuishi siku zaidi
Unyanyasaji/Udunishaji wa Wanawake na Utamaduni/Taasubi ya Kiume
- Kutorithi mali
- Wanawake wajane kunyang’anywa mali na kufukuzwa
- Ndoa za wake wengi (uke wenza)
- Kupata watoto wengi
- Kurithi wanawake
- Kupashwa tohara
- Kutawishwa au kunyimwa uhuru wa kutoka
- Kutoelimishwa eti kwa akiolewa hatafaidi familia, atapanda wanaume vichwa au atakuwa malaya
- Ndoa za mapema/lazima zinazosababisha kukatiza elimu yake (mahari haiwezi kurudishwa)
- Kulazimishwa kuolewa na mtu asiyempenda
- Kunyimwa haki ya kusema
- Kupigwa na kutusiwa
- kubakwa
- Kutalikiwa
- Wanaume kutokuwa waminifu kwao hata kuwanyima mahitaji na kuwapa mahawara zao
- Wanaume kupuuza majukumu ya kukimu familia
- Ubadhirifu wa wanaume na hali wake zao ndio walifanya kazi za kupatia hizo pesa
- Kubughudhiwa
- Kulaumiwa mtoto akikosekana hata mke mwingine kuolewa
- Mahali pa mwanamke kuwa nyumbani au haruhusiwi kufanya kazi ofisini au kuongoza
- Kulazimishwa kuvaa mavazi aina fulani na kukatazwa kuvaa aina mengine
- Kufanyishwa kazi za nyumbani kama mtumwa
- Kudhibitiwa na wanaume zao kwa sababu ya vivu.
- Kunyimwa ajira kwa vile akipata mimba atajikokota kazini na atahitaji likizo baada ya kujifungua.
- Ajira ya mtoto wa kike ambapo anafanyishwa kazi ya sulubu na kupewa mshahara duni
Suluhisho
- Hatua kali za kisheria kwa wanaowapiga, wanaowabaka na wanaotekeleza mila ya tohara na ndoa za mapema
- Kufanya kampeni dhidi ya mila zinazochangia udunishaji wa wanawake
- Kuwashauri watoto wa kike badala ya kuwapasha tohara
- Kuanzisha makao ya watoto wa kike wanaotishiwa na mila mbaya
- Kumwelimisha mwanamke kuhusu haki zake
- Kuhimiza wanawake kupigania haki zao
- Serikali kutenga pesa za kuelimisha watoto wa kike ili kuwapa uwezo wa kiuchumi kwani wengi hunyanyaswa kutokana na umaskini na ujinga.
- Mashirika ya kutetea haki za wanawake kama FIDA na Maendeleo ya Wanawake.
- Hazina ya kutoa mikopo kwa makundi ya wanawake k.v. K.W.F.T
- Kuwapa wanawake nafasi sawa za ajira na katika uongozi.
- Kupunguza alama ambazo wasichana wanazopaswa kufikisha ili kujiunga na vyuo vya elimu ya juu.
- Kubuni sheria za kuwawezesha kumiliki mali
Jinsi Wanaume Wanavyodhulumiwa
- Kupigwa
- Kuchomwa kwa maji moto
- Kukatwa sehemu nyeti
- Wanawake kutokuwa waminifu kwao
- Kutusiwa
- Kutofuliwa nguo
- Kunyimwa chakula
- Kunyimwa unyumba kama njia ya kulipiza kisasi au kumwadhibu
- Kufanyishwa kazi fulani k.v. kufulishwa nguo na kupikishwa mke akiwepo hata mbele ya wageni
- Kuzomewa/ kugombezwa
- Kunyimwa pesa kama hana ajira
Ufisadi
- Uovu, ubaya au uharibivu.
Aina
- Wanafunzi kudanganya katika mtihani
- Kufanyiwa mtihani na watu wa nje
- Kutoza mwanafunzi wa kidato cha kwanza pesa au chakula kama nyama ili kuwalinda.
- Kujipakulia chakula kingi.
- Waalimu wakuu kuitisha hongo ili kuruhusu wanafunzi wajiunge na shule zao
- Kupita wengine katika foleni wanapokwenda kupata chakula au chai hata benki
- Kurudishiwa bakaa/chenji nyingi dukani na kutoirejesha kwa muuza duka.
- Kuokota pesa njiani na kutoulizia ni za nani
- Kughushi stakabadhi za mtihani, hati za umiliki shamba
- Kunakili kanda za muziki za wengine na kuziuza
- Waajiri kuajiri watu wa familia zao au makabila yao
- Daktari kuitisha hongo ili amhudumie mgonjwa
- Polisi kuitisha hongo ili aruhusu magari ya huduma kwa umma yasiyofaa kupita
- Kutohoa maziwa au kuyaongezea maji ili yawe mengi
- Wenye maduka kuuza bidhaa kwa bei ghali
- Kuuza bidhaa kama sukari, nyama, nafaka, gesi na mafuta ya petroli ambazo hazijatimiza uzani unaotakikana
- Madereva wanaoendea mafuta ya petroli kuuza kiwango fulani cha hayo mafuta na kuongezea ya taa au diseli
- Kuuzia watu dawa bandia zisizotibu magonjwa
- Ulanguzi wa dawa za kulevya
- Kuiba pesa kwa kutumia risiti bandia au kufuruisha bei za bidhaa ili pesa zilizo juu wahusika wagawane
- Kutoa ushahidi wa uongo
- Kunyang’anya wajane na yatima mali zao
- Uporaji wa mali ya umma k.v. nyanja za kuchezea watoto na misitu
- Hakimu kuchukua hongo aididimize kesi
- Madaktari kutoza wawele ada ya juu hata kuwafanyia upassuaji wasiouhitaji ili wapate pesa.
- Wafanyakazi wa halmashauri za miji kujificha wanapomwona mtu akiegesha gari ili wadai anakwepa kulipa ada ya uegeshaji ili wahongwe au walikokote gari wapate pesa zaidi.
Sababu Ya Watu Kuushiriki Ufisadi
- Tamaa ya kutajirika
- Kutofahamu madhara/matokeo yake
- Kukosa njia za kukimu mahitaji
- Mishahara au mapato duni yasiyomwezesha mtu kukimu mahitaji yake au ya familia
- Kutotosheka kwa kile mtu alichonacho
- Hofu ya kupata hasara au kukosa ajira
- Kutomjua mungu hivyo hawana imani
- Kuzugwa au kutekwa nyara kimawazo na kuwa mtumwa na shetani
- Wengine hulichukulia kama jambo la kawaida tu au hali ya maisha
- Imani kuwa siku hizi mtu hawezi kupata chochote bila kutoa hongo
Madhara
- Vifo kutokana na aajali barabarani au kutotibiwa bila hongo
- Majeruhi wa ajali za ajalini wengine hulemaa wasiweze kujifanyia kazi zao
- Kufutiliwa kwa matokeo ya mtihani
- Kufukuzwa shuleni au chuoni
- Umaskini kutokana na utoaji hongo ya pesa nyingi kisha kutopata kazi na ununuzi wa bidhaa kwa bei ghali
- Kushuka kwa viwango vya elimu wasiohitimu ipasavyo wanaporuhusiwa kujiunga na shule ama vyuo fulani
- Kushuka kwa viwango vya huduma kwa umma kutokana na kuajiriwa kwa watu ambao hawajahitimu vizuri.
- Afisi za serikali kuchomwa wafisadi wakijaribu kusitiri ushahidi wa ufisadi
- Nchi kurudishwa nyuma kiuchumi na kimaendeleo kutokana na pesa za miradi au ambazo zingewekezwa katika vitega uchumi kuporwa
- Kupoteza ajira baada ya kufutwa kazi kutokana na ufisadi
- Familia kuteseka baada ya kupoteza ajira
- Kufungwa jela kwa wanaopatikana na kosa la ufisadi
- Uharibifu wa mazingira na madhara yanayoendana nao kutokana na ufyekaji wa misitu
- Kudidimiza haki pale kesi inakatwa vibaya kutokana na hongo hata asiye na makosa aweza kufungwa
- Viongozi wafisadi katika mashirika na asasi kupoteza nyadhfa
Suluhisho/Njia za Kuukabili Ufisadi
- Hatua kali kisheria kwa wafisadi
- Kulipa wafanyakazi mishahara mizuri
- Kuelimisha kuhusu madhara ya usisadi
- Kufuta kazi wafisadi
- Kunyang’anywa pesa au mali walizopata kifisadi
- Watu kutangaza mali zao k.v. kwa kujaza fomu kudhihirisha hayo
- Shirika la kukagua vipimo na ubora wa bidhaa
- Majina ya wafisadi kutangazwa hadharani
- Ukaguzi wa hesabu za matumizi ya pesa katika asasi za serikali
- Shirika la kupambana na ufisadi
- Kufumania wafisadi
- Kupiga picha kwa kamera ya video wafisadi k.v. polisi wakichukua hongo
- Kujifunza kutosheka kwa kile mtu alichonacho na kuishi maisha ya kiwango chake.
- Kuarifu polisi au shirika la mkupambana na ufisadi kuhusu visa vya ufisadi
- Kumjua na kumcha Mungu
Dawa za Kulevya/Mihandarati
- Dawa ambazo huathiri utendakazi wa mwili.
Sababu za Kutumiwa
- Masurufu au kuwapa vijana pesa nyingi za matumizi
- Kujipa burudani
- Shinikizo la rika kwa vijana
- Ukosefu wa ushauri/kutojua madhara
- Matangazo ya biashara
- Shida k.v. ukosefu wa ajira na mahitaji ya kimsingi
- Marafiki wabaya
- Kukaa katika mazingira zinamotumiwa
- Malezi
- Kuvunjika kwa ndoa
- upweke
- Kujitoa haya k.m. makahaba
- Shida kazini
- Kudanganywa zina manufaa k.m. kumpa mtu nguvu ya kufanya kazi au kuerevusha
- Kujipa hisia za kuwa huru na ujitambuaji
Madhara
- Magonjwa k.v. saratani na ya zinaa
- Vifo kutokana na ajali, magonjwa au dawa zenyewe
- Kuiba ili kupata pesa za kununulia dawa za
- Ubakaji
- Hufilisi watu kwa kutumia pesa nyingi hata kuuza au kuzikodisha mali zao ili kuzigharamia
- Jamaa kuathirika kisaikolojia wanapoona mwenzao akiKushindwa kuendelea na masomo.
- Visa vya ubakaji.
- Kupotoka kimaadili k.m. kuwa mwenye matusi, kupiga wengine, kuwa mgomvi hata mzinifu.
- Kuwa mchafu kama fungo k.m. kutooga, kutofua nguo, kutochanua nywele n.k.
- Kuhisi mambo yasiyokuwepo (hallucination).
- Wengine kushindwa kuolewa na kutoweza kupata watoto k.m. watumiaji wa miraa.
- Kuvunjika kwa ndoa kutokana na kupiga mke, kutumia pesa vibaya.
- Kufutwa kazi k.m. kutokana na ulevi.
- Wazimu
- Uhalifu
- Jamaa ya mtumizi kuteseka ikimwona mwenzao akiangamia kutokana na kuzitegemea dawa za kulevya
- Mhusika huathirika kimwili na kisaikolojia
- Huathiri ukuaji wa mwili na akili
- Wazimu
- Huathiri uwezo wa kufikiri kwa kuua seli za ubongo
- Hufanya mtu kupotoka kimaadili k.m. upyaro, vita, uchoyo, uzinifu
- Kuvunjika kwa ndoa
- Kufukuzwa shuleni
- Kufungwa jela
- Kuzaa watoto ambao hawajatimiza uzani wa wastani
- Kufa kwa neva na viungo kukatwa
Suluhisho
- Kuelimisha watu kuhusu madhara ya dawa za kulevya
- Watu kumjua Mungu
- Matibabu ya kurekebisha watumwa wazo
- Kujitenga na marafiki wabaya
- Kutoingia katika mandhari zinamotumiwa
- Maelekezo kuhusu dawa za matibabu kufuatwa ipasavyo
- Kutotumia dawa za matibabu kwa matumizi mengine yasiyo ya kutibu
- Ukaguzi wa wageni na mizigo katika viwanja vya ndege
- Hatua za kisheria kwa walanguzi, wauzaji na watumiaji
- Kuongeza nafasi za ajira
- Kukomesha matangazo ya biashara ya dawa hizo
- Kuandika matahadharisho katika chupa na pakiti za vileo
Uhalifu/Utovu wa Usalama
Chanzo
- Umaskini kusababisha wizi na uisadi
- Dawa za kulevya kusababisha wizi au kubaka
- Marafiki wabaya
- Malezi mabaya
- Malezi mabaya k.m. mtoto akiiba na kupelekea wazazi, wazazi hawamuulizi alikotoa vitu hivyo.
- Tamaa ya mali kufanya watu kuiba, kushiriki ufisadi, n.k.
- Hasira au kushindwa kujidhibiti kusababisha kumpiga na kumuumiza mtu hata kumuua
- Tamaa kubwa au uchu kusababisha ubakaji.
- Chuki na wivu huweza kusababisha mauaji
Suluhisho
- Hatua kali za kisheria
- Kuongeza askari kwani idadi yao ni dogo ikilinganishwa na raia
- Kuunda vikundi vya kujilinda
- Vituo vya polisi kuongezwa
- Vitu vya thamani kuwekwa mahali salama k.m. benki
- Kutotembea nyakati za usiku
- Kutoendea mahali kusikofaa k.v. vichochoroni
- Kuweka ua na lango
- Mavazi yanayofaa kuzuia ubakaji
- Kutoa mafunzo ya kujikinga
- Nambari za simu za dharura za kuripotia uhalifu
- Kumjua Mungu
- Kuongeza nafasi za ajira
Haki za Binadamu
- Kuishi
- Kuingiliana/kutangamana
- Uhuru na usawa
- Elimu
- Makazi
- Afya
- Kiwango cha kurithisha cha maisha
- Chakula
- Kuabudu
- Ajira ya watoto
- Kufanya kazi
- Kumiliki mali
- Kutunzwa uzeeni/ hifadhi ya jamii/wasio na uwezo
- Kupiga kura
- Kutobaguliwa
- Kutoteswa kuminya habari
- Uhuru wa kuongea/usemi
- Kutembea na kuishi popote
- Kesi kuendeshwa kwa haki
- Kujitetea
- Kuoa au kuolewa na unayemtaka
- Utulivu k.m. mtoto au mke asipigwe ama kuteswa
- Huduma za matibabu
- Jina na utaifa wakati wa kuzaliwa
- Mtoto mlemavu apewe huduma maalum
- Alindwe kutokana na mateso, kazi ya sulubu na kuhusishwa vitani
- Alindwe dhidi ya mila na tamaduni zisizofaa
- Haki ya kupata burudani
- Haki ya faragha/ kuhifadhi siri zake
- Asiajiriwe
- asiteswe
Jinsi ya kuwalinda na kuwatunza watoto
- Sheria kubuniwa za kuwalinda
- Hatua kali kisheria kwa wanaodhulumu watoto
- Shirika la kupigania haki za watoto
- Makao ya watoto wanaokimbia wa dhuluma
- Hazina ya wizara na maeneo bunge ya kufadhili watoto maskini (bursary)
- Watoto kuelimishwa kuhusu haki zao
- Kuelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa kulinda mtoto
- Elimu ya bure ili watoto maskini wafaidi
- Shule maalum kwa watoto walemavu
- Wananchi kuchanga kusaidia watoto maskini
- Makanisa kusaidia watoto yatima
- Shule kuwapa watoto maskini ufadhili
Mazingira
- Hali au mambo yanayomzunguka kiumbe katika sehemu anakoishi.
Jinsi Yanavyoharibiwa
- Kufyeka misitu ili kupata mahali pa makazi ama kulima
- Kufuga mifugo kupita kiasi
- Kutupa taka ovyoovyo
- Moshi kutoka katika magari na viwanda huchafua hewa
- Dawa na mbolea za kemikali za kilimo huchafua udongo na maji.
- Migodi kuacha mashimo ardhini ambayo hujaa maji na kuwa hatari kwa binadamu na kizalio cha mbu.
- Kelele za vyombo vya mziki, viwanda, honi za magari na ndege
- mafuriko kuchanganya choo pamoja na maji safi
- Taka kutoka nyumbani na viwandani kuelekezwa mitoni.
Madhara
- Ongezeko la joto duniani
- Mvua za gharika
- Uhaba wa mvua
- Ukame na njaa
- Uhaba wa maji
- Kufa kwa wanyama wa majini kama samaki
- Magonjwa na vifo kutokana na kuathiriwa na maji machafu
- Magonjwa ya mapafu kutokana na hewa chafu
Suluhisho
- Kupanda miti kusiko na miti na kule misitu imefyekwa
- Elimu kuhusu madhara ya kuharibu mazingira na jinsi ya kuyatunza Uhaba wa maji.
- Kukagua viwabda na hatua za kisheria kama vinavyoachilia taka katika mazingira
- Kutumia samadi badala ya mbolea za kemikali na dawa za kiasili kuua wadudu katika mimea na mifugo
- Kutaifisha misitu
- Askari wa kulinda misitu
- Kutumia kawi mbadala na ambazo hazichafui mazingira k.v. kutokana na maji na jua
- Mashimo na mapipa ya kutupa taka
- Kuweka mifugo kulingana na eneo la malisho
- Kutolima kando ya mito
- Kutia choo cha binadamu dawa kabla ya kukiachilia mitoni
- Kutumia magari ya umma
- Kutumia taka kama malighafi na kutumia vile vitu vyaweza kutumika tena
Usalama Barabarani
Vyanzo vya ajali
- Madereva kutohitimu vizuri
- Magari mabovu
- Kutotii sheria za barabarani
- Njia mbovu
- Kubeba abiria na mizigo kupita kiasi
- Kuendesha magari kwa kasi
- Waabudu shetani kusababisha magari kupoteza mwelekeo
- Kupita magari mengine bila uangalifu
- Ulevi
- Wenda miguu kutokuwa waangalifu wanapovuka barabara
- Kutodhibiti usukani vizuri
- Uchovu kusababisha usingizi
- Dawa za matibabu
- Abiria kutolalamika au hata kumwambia dereva aendeshe kwa kasi wafike haraka
- Kuchanganyikiwa
Suluhisho
- Hatua za kisheria kwa wakiukaji kanuni za barabarani
- Kuondoa polisi wafisadi barabarani
- Kukarabati barabara
- Ukaguzi wa magari ili kuhakikisha yafaa kuwa barabarani
- Kufunza madereva upya
- Mikanda au mishipi ya kujifunga kuzuia kujeruhiwa vibaya na vifo ajali ikitokea
- Kuweka vidhibiti mwendo
- Vifaa vya kutambulia madereva walevi na kasi ya magari
- Uangalifu wakati wa kupita magari mengine
- Kuwa mwangalifu wakati wa kuvuka barabara
Sayansi na Teknolojia
- Uvumbuzi wa umeme unaotumiwa kuangazia na kuendesha vyombo vingi
- Matibabu kuwezesha watu kuishi kwa muda mrefu k.m. dawa,chanjo, upasuaji, upachikwaji viungo, miale ya kutibu saratani, n.k.
- Kurahisisha na kuharakisha usafiri k.m. magari, pikipiki, ndege, k.m.
- Kurahisisha na kuharakisha mawasiliano kunakosaidia wakati wa dharura k.m. rununu, mtandao, nukulishi, n.k.
- Upashaji wa habari kuwezesha kupata habari kutoka kote duniani k.m. satalaiti, mtandao, redio, runinga, n.k.
- Utengenezaji bidhaa viwandani kuharakishwa kutokana na mitambo inazoendesha na tarakilishi
- Mimea na mifugo wanaokomaa haraka na walio na mazao mengi
- Roketi inayowezesha kwenda katika mwezi na sayari nyingine
- Silaha kama bunduki za kupambana na maadui na wahalifu
- Burudani bora k.m. sidi, video, mtandao, n.k.
Madhara
- Uavyaji mimba
- Mauaji ya huruma
- Tishio la dunia kuangamia kutokana na silaha za nuklia na viini vinavyotengezezewa maabarani
- Uhalifu kuongezeka kutokana na wingi wa bunduki, simu na mtandao
- Vyakula kutokana na mimea ina mifugo iliyokuzwa kisayanzi kudhuru afya
- Wizi wa viungo vya mwili hata kuhasiwa bila hiari
- Ajali za barabarani na za ndege zinazoua watu wengi
- Upotoshaji kimaadili kama vile filamu chafu katika mitandao na sidi
- Kutumia vijusi kutengenezea viungo
- Ongezeko la joto duniani kutokana na uchafuzi wa hewa
- Ugaidi kutokana unaotekelezwa kwa mabomu
Simu za Rununu
Faida
- Kurahisha na kuharakisha mawasilano
- Kupunguza gharama za usafiri
- Mtandao huelimisha na hufahamisha habari
- Kutuma pesa
- Kuweka pesa/akiba
- Burudani k.m. nyimbo, michezo
- Kupiga nduru uhalifu unapotokeo
- Ajira kwa wauzaji na watengenezaji
- Ushuru kwa serikali
- Shajara, kalenda, kamera, kikokotozi
Madhara
- Burudani kusababisha ajizi
- Uhalifu
- Gharama kubwa hasa kuweka chaji na malipo kabla ya kutumia kuongea au mtandao
- Mtandao kupotosha kimaadili
- Hutoa miale ambayo yaweza kusababisha saratani
- Kudanganya katika mitihani
- Kufungwa jela kutokana na arafa za vitisho na matusi
Runinga/magazeti
- Burudani
- Habari
- Ajira kwa wanahabari na watangazaji
- Matangazo ya biashara
- Kufunza maadili k.m. michezo ya kuigiza na vichekesho.
- Kutuwezesha kufahamu sehemu nyingine za nchi na dunia
- Kuelimisha k.v. vipindi vya fasihi
- Utalii
- Kuangazia sehemu na watu wenye shida
- Kukuza lugha
- Kukuza uzaleno
Madhara
- Ajizi
- Kupotosha kimaadili
- Filamu ziazohimiza watu kuwa wazinifu.
- Matangazo ya vileo
- Kuenezea chuki na propaganda
- Kuiga utamaduni wa kigeni usiofaa k.v. mavazi, talaka
- Gharama ya kununulia
- Kutopata muda wa kushauri watoto na kuomba
- Wanafunzi kutosoma jioni
- Mke na mume kutoongea kujadili mwelekeo wa familia
- Wanaume kuchelewa kurudi nyumbani usiku wakitazama mpira
- Migogoro kwa kutaka kutazama vipindi tofauti
- Kelele na usumbufu kwa waliolala
Utalii
- hali ya kusafiri mbali ili kuvinjari au kufurahia mandhari
Faida
- Fedha za kigeni
- Ajira katika hoteli, udereva, n.k.
- Uhifadhi wa mazingira
- Kuboreshwa kwa miundo msingi
- Mapato kwa serikali kutokana na ada ya kuingilia mbugani na kodi za mikahawa
- Amani na maelewano nchini na duniani
- Kuhifadhi mila na tamaduni zetu
- Kupa nchi umaarufu duniani
- Maeneneo kame kuweza kutumiwa ipasavyo kama kivutio chao
- Soko kwa mazao ya kilimo
- Kuwapa wauzaji vinyago mapato
Ubaya
- Magonjwa k.v. ya zinaa
- Matumizi ya mihandarati
- Tabia zisizofaa k.v. Usenge zinazovunja ndoa na kueneza magonjwa kama ukimwi
- Upuuzaji wa miradi ya maendeleo serikali ikijengea watalii hoteli za kifahari na viwanja vya ndege ambavyo hutumika kwa nadra sana
- Kusababisha watoto kuacha shule ili wawe wanawaelekeza wapate pesa
- Kuhimiza mauaji wa wanyama kwa kununua pembe na ngozi
- Kelele za magari yao husumbua wanyama na kukanyaga na kuharibu lishe yao
Jinsi ya kuvutia watalii zaidi
- Kudumisha usalama
- Kuimarisha miundo msingi
- Kutangaza nchi na vivutio nje
- Kupunguza malipo katika hoteli za watalii
- Kufahamisha wananchi kuhusu vivutio kupitia vyombo vya habari
- Kuongezea wafanyakazi mishahara ili kuweka akiba waweze kuzuru maeneo yenye vivutio
- Kuwapa wafanyakazi likizo ya kutosha
Umaskini
Suluhisho
- Kuongeza nafasi za ajira
- Kutoa mikopo rahisi kulipa
- Kupunguza bei ya pembejeo
- Elimu ya bure
- Kupigana na ufisadi
- Upangaji uzazi ili kupunguza idadi ya watu
- Bei bora ya mazao ya kilimo
- Kazi kwa vijana
Ukeketaji
Sababu
- Kupunguza tamaa
- Njia ya kukomaa
- Mila na tamaduni
Madhara
- Kifo kwa kutokwa na damu sana
- Uenezaji wa magonjwa
- Shida wakati wa hedhi na kujifungua
- Ndoa kuvunjika
- Kibali cha kujiingiza katika myenendo isiyofaa
- Utengano kati ya waliotahiriwa na ambao hawajatahiriwa -migogoro
- Kuzua utabaka baina ya waliopashwa na wasiopashwa tohara
Suluhisho
- Hatua za kisheria
- Elimu kuhusu madhara
- Mawaidha kwa wasichana
- Makao ya watoto
Njaa
- Kilimo cha unyunyizaji maji
- Kupunguza bei za pembejeo
- Njia bora za kuhifadhi mazao
- Mimea na mifugo inayokomaa haraka
- Utumizi wa samadi na mbolea
- Kuelimisha wakulima kuhusu kilimo bora
- Kutayarisha mashamba mapema
- Serikali kununua mazao ya wakulima na kuyahifadhi
Dini
Uzuri
- Kufunza maadili
- Kusaidia maskini
- Kuanzisha shule na hospitali
- Ajira kwa padri, kasisi n.k.
- Kuandaa watu kwa maisha baada ya kifo
- Kufariji/kuliwaza wenye dhiki
Ubaya
- Tamaa ya pesa
- Biashara
- Ubakaji wa watoto
- Kuuza uponyaji
- Nyingine kutosaidia wenye shida
- Vita/jihadi
- Kuruhusu waovu bora watoe pesa
- Kutoenda hospitalini
- Kuendeleza maovu k.v. uzinifu, ushirikina, uabudu shetani, n.k.
Maasi ya vijana
- dawa za kulevya
- shiniko la kikundi
- filamu mbaya
- kudhibitiwa kupita kiasi
- kukosa nidhamu
- malezi mabaya/udekezaji
- kubomoka kwa msingi wa jamii
- Ufukara kusababisha kujiunga na makundi haramu
- Kukata tamaa
- Kutumiwa vibaya na wanasiasa
Suluhisho
- Kujiondoa kundini
- Kuimarisha uchumi
- Kuwashauri vijana
- Kujenga udhabiti wa jamii
- Kuwaadhibu kulingana na makosa yao
- Vijana kujisaka na kujikosoa
- Vijana kumjua mungu
- Uhuru wa kadiri
- Uongozi bora
- Malezi bora
- Kuongeza nafasi za ajira
Umoja na Utangamano katika Familia
- Kuheshimiana
- Utiifu na unyenyekevu
- Kuwa na usemi
- Kuvumiliana na kusameheana
- Uaminifu na kuaminiana
- Kutochagulia watoto taaluma na wachumba
- Wazazi kutolazimisha watoto taaluma au kozi wasizotaka
- Kutumia pesa vyema bila ubadhirifu
- Kutopendelea na kulinganisha watoto kiuwezo
- kutotumia dawa za kulevya
- Kuomba pamoja
- wazazi kutopendelea watoto fulani
- Baba kutimiza majukumu yake ya kukimu jamii
- Kutodhibiti mke na watoto kupita kiasi
- Uadilifu
- Kushiriki kazi
Mambo yanayoathiri utaifa/umoja na utangamano/amani
- Ufisadi k.v. kuajiri watu kimapendeleo
- Ukabila
- Viongozi kueneza chuki
- serikali kutoakisi uwakilishaji wa taifa zima
- Usalama kukosekana
- Ukosefu wa ajira
- Matamshi mabaya ya viongozi
- Kupanda kwa gharama ya maisha
- Majanga ya kiasili
- Kutojenga miundo msingi kwa usawa
- Kupendelea maeneo fulani katika ugawaji wa raslimali
- Ukimbizi wa ndani kwa ndani
- Ubomoaji wa nyumba
Suluhisho
- Lugha ya taifa
- Kukabiliana na ufisadi
- Usawa katika ugawaji wa raslimali
- Kuelimisha kuhusu umoja wa kitaifa
- Tamasha za kitamaduni
- Kutalii sehemu nyingine za nchi
- Ndoa za makabila tofauti
- Serikali ya muungano
- Viongozi wachochezi kuchukuliwa hatua kisheria
Matatu
Faida
- Kurahisisha na kuharakisha usafiri
- Ajira
- Ushuru
- Biashara
- Huduma za dharura
Madhara
- Ajali
- Wizi
- Ufisadi wa polisi kuongezeka
- Kuongeza nauli ghafla
- Ujeuri wa madereva na mataniboi
- Kuchelewesha watu njiani
Magazeti
- Habari za taifa na kimataifa
- Kuelimisha k.m. kuhusu afya
- Kuburudisha k.m. vibonzo
- Matangazo ya biashara
- Ajira k.m. wahariri, wauzaji
- Mapato kwa serikali
- Kutangaza nafasi za ajira
- Elimu k.m. uchambuzi wa vitabu vya fasihi na mashairi
- Hutumiwa kufungia bidhaa
Ubakaji
- Sura mbaya
- ulevi
- Ulemavu
- Unyonge wa kiakili
- Kushindwa kudhibiti jicho na tamaa za mwili
- Njaa ya kimapenzi
- Kisasi
- Kujihisi duni
- Kisomo duni
- Mavazi
Athari
- Waliobakwa huathirika kisaikolojia
- Kujikosea heshima na kujihisi mchafu
- Magonjwa ya zinaa
- Mimba zisizotakikana
- Vifo
- kujeruhiwa
- Kupoteza imani na wanaume/wanawake
- Kutengwa
- Kufungwa jela
3. UTUNGAJI WA KISANII
- Mashairi mepesi (huru/arudhi)
- Hadithi fupi
- Vitendawili
- Mafumbo/chemshabongo
- Vitanza ndimi
- Michezo ya kuigiza
Mambo ya Kuzingatia katika Uadishi wa Insha
- maagizo
- Usijibu swali usilolielewa
- Uandishi mzuri wa nambari ya swali unalofanya
- Kuandika vidokezi
- Kuandika kila hoja katika aya yake
- Kuanzia aya kwa njia tofauti
- Lugha sahili
- Miundo tofauti ya sentensi
- maudhui
- muundo
- Kichwa kwa herufi kubwa, kipigwe mstari na kisizidishe maneni sita
- Upatanisho/uwiano za kisarufi
- Tahajia/hijai
- Kuakifisha
- Mtiririko
- Uhalisi
- tafsiri ya moja kwa moja k.m. kurudisha mlango, mguu wa gari, kutoa/kuweka nguo
- Maadili (lugha na mawazo safi na mtazamo wa kusaidia taifa)
- Urefu
- Uasilia (utungo wako si kurejelea vitabu vya fasihi)
- Usafi (mwandiko unaosomeka na ambao haujapigwapigwa mistari na kufutwa)
- Tamathali za usemi
- Msamiati na tamathali zinazokubalika wala si za kupachika. Usitumie msamiati wa kishairi k.v. mtima, ja, n.k.
- Kutofupisha k.v. k.m., n.k., Bi.
- Kutumia kistari ikiwa neno linaendelea katika mstari wa pili na kutokata silabi
- Herufi f, u, i, j, m, l
- Kutaja na kueleza kikamilifu
- Kukamilisha maneno
- Kutotenganisha sehemu za neno k.m. walilo zungumzia, walioenda
- Kutounganisha maneno k.m. kwasababu, ni mimi
- Mdokezo kuoana na maneno yako.
- Usiongeze maneno kwenye dondoo la kumalizia.
- Kutoweka dondoo ni kupotoka
- Kusoma insha baada ya kuandika
4. UANDISHI WAKAWAIDA
Ufahamu
- Kuelewa
- Kuandika idadi ya hoja kulingana na alama
- Hoja kwa muhtasari
- Andika hoja ulizo na uhakika nazo kwanza
- Kuorodhesha hoja kwa nambari wala si kistari
- Jibu lililokamilika
- Kutoa majibu kutoka katika ufahamu si fikra zako
- Maana za maneno kama yalivyotumiwa kwa muundo ule ule
Muhtasari/Ufupisho
- Kutoa mawazo makuu huku kiini cha taarifa kikidumishwa.
Hatua
- Andika nambari za aya
- Soma makala
- Elewa swali
- Andika mambo muhimu ukizingatia swali ukiondoa maneno yasiyo muhimu
- Usibadilishe chochote hata kama unatakiwa kutumia maneno yako
- Andika hoja kikamilifu
- Andika nakala safi ukizingatia mtiririko
- Epuka viunganishi vingi
- Zingatia idadi ya maneno uliyopewa
- Zingatia kanuni za uandishi
- Piga mshazari nakala chafu
Matumizi ya lugha
- Kuzingatia sehemu za swali
- Sehemu zinazobadilika
- Kuzingatia neno moja moja
- Kuzingatia hatua au mbinu
- Kutojibu maswali kwa pupa
- Kusoma jibu ili kusahihisha makosa
- Kuelewa swali k.m. tunga sentensi moja, eleza maana
- Tunga sentensi fupi
- Kuonyesha neno, fungu la maneno au kiambishi unachotumia kutunga sentensi
- Kubainisha (eleza kikamilifu kwa kuandika neno au maneno na jina lake)
- Tahajia k.m. yabwa, kitendo
Isimu jamii
- Kutaja, kueleza na kutoa mifano
Fasihi
- Kufikiri ili kuelewa swali
- Usijibu maswali zaidi ya manne. Kama jibu halikuridhishi, lipige mshazari
- Maagizo (swali la kwanza ni la lazima, usijibu maswali mawili kutoka sehemu moja
- Chagua maswali utakayoweza kujibu na kupata hoja nyingi
- Andika nambari vizuri
- Usiandike hoja nyingi kuliko alama
- Andika hoja ulizo na uhakika nazo kwanza
- Hoja kwa aya moja
- Kutaja, kueleza kikamilifu na kuthibitisha kwa mifano kutoka kitabuni (kutaja alama moja, kueleza mbili)
- Usirudie hoja kwa njia tofauti
- Kutochanganya wahusika
- Kusoma vitabu mara nyingi ili kujua dondoo limetolewa wapi
- Maswali ya dondoo (msemaji, anayeambiwa, wapi, lini)
- Maswali ya kujadili
- Swali la methali
- kulinganisha
- Andika nambari za aya


2 Comments