Share this:
Maswali ya Hadithi Fupi : K. WAMITILA: MAYAI WAZIRI WA MARADHI NA HADITHI NYINGINEZO
1. Ukirejelea mkusanyiko wa hadithi fupi: Mayai Waziri wa Maradhi na Hadithi Nyingine,
Onyesha msimamo wa mwandishi Rayya Timammy kuhusu kura na uongozi.
2. K. Wamitila anatumlikia jamii iliyojaa uozo wa kila aina. Eleza kauli hii kwa kurejelea diwani
ya Mayai Waziri wa Maradhi na Hadithi Nyingine.
3. “Euphrase Kezilahabi ni mwingi wa Jazanda na Ndoto katika uandishi wake.” Thibitisha
kauli hii kwa kurejelea hadithi ya Mayai waziri wa maradhi.
4. “Hii ni dunia ya dua la kuku halimpati mwewe!” Alijiambia. Baada ya muda aliongeza “anayepanda juu kipungu hafikili mbinguni.”
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili
b) Ukirejelea hadithi ya Msamaria Mwema, onyesha vile hii dunia ni ya ‘Dua la kuku
5. Soma makala haya kisha ujibu maswali
Angeko, Angeko ee
Angeko, Angeko ee
Ni kilio, Kilio ee
Ni kilio, kilio ee
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
(b) Eleza mbinu ya uandishi iliyotumiwa kwenye dondoo hili.
(c)Eleza matukio ya kweli ambayo mtunzi ameyaangazia katika hadithi. “Ndimi za mauti”.
6. Kwa kurejelea hadithi ya Mkimbizi eleza madhara ya vita
7. Sote tulisimama ghafla kama tumesimikwa ardhini”. Huu mwisho wetu sasa!”
(a) Fafanua muktadha wa maneno haya
(b) Taja na ueleze mbinu ya lugha ambayo imetumiwa katika muktadha huu
(c) “Nilikumbuka ile sura ya mama na ndugu zangu”. Ni kwa nini msemaji anawakumbuka
mama na ndugu zake?
(d) Eleza matatizo yaliyowakumba wakimbizi kulingana na hadithi
(e) Eleza maudhui yanayoibuka katika muktadha
8. Jadili wahusika wafuatao na dhima yao katika hadithi ya Fumbo la mwana :
i) Makulu
ii) Mwalimu
iii) Mzee Atanasi
9. (a) Kwa kurejelea hadithi za Mkimbizi na Fumbo la Mwana, eleza jinsi ambavyo mchafuko
wa kisiasa na matumizi ya dawa za kulevya zinavyoweza kuzorotesha ukuaji wa jamii
(b) Kwa kurejelea hadithi za Uteuzi wa Moyoni na Ngome ya Nafsi, eleza jinsi haki za
wanawake zilivyokiukwa
10. “Unavyoona ni kama aligongwa…..basi mimi nikamkuta pale anagaragara chini. Unajua zamani
nikienda kanisani.. nakumbuka kisa cha Msamaria ; kufupisha habari mimi ni Msamaria mwema
niliyemwokota mzee huyu chini.”
(a) Ni nini kilikuwa kimetendeka ili dereva ayatamke haya ?
(b) Ingawa Dereva alijiita msamaria mwema, ni yapi hakuwa tayari kufanya masamaria
mwema aliyoyatenda katika Bibilia ?
(c) Unafikiri ni ni kilichosababisha ajali ndiposa mzee huyu agongwe ?
(d) Onyesha vitendo vya ‘Msamaria Mwema’ vinavyoelekea kuthibitisha kwamba ndiye
aliyemgonga mhasiriwa
11. Mbinu ya majazi na mbinu rejeshi hutumiwa na waandishi wengi ili kuwasilisha ujumbe wao.
Huku ukitoa mifano kutoka hadithi mbalimbali thibitisha ukweli wa kauli hii
12. Utamaduni unaomkandamiza mwanamke umetamalaki katika jumuiya ya hadithi za Uteuzi
moyoni na ‘Ngome ya Nafsi’. Kwa kurejelea hadithi hizi, eleza jinsi utamaduni umetumiwa
kukandamiza wanawake
13. Diwani ya Mayai Waziri wa Maradhi imejikita katika masuala ibuka yanayofaa kushughulikiwa
na jamii. Taja na uthibitishe.
14. Fafanua dhamira ya Ken Walibora alipoandika kisa cha “Tuzo”
15. “Mara nyingi vijana hushughulikia mambo ya kibinafsi. Mara nyingi mawazo yao
hufuata mkondo wa anasa za vijana tu.”
(a) Eleza muktadha wa usemi huu.
(b) Onyesha ushahidi wowote katika tamthilia kudhihirisha ukweli wa kauli hii.
(c) Fafanua mambo waliyofanya vijana katika tamthilia kuonyesha kuwa walipigana kwa
niaba ya umma.
Majibu ya Hadithi fupi K. WAMITILA: MAYAI WAZIRI WA MARADHI NA HADITHI NYINGINEZO
1.
- Mwandishi namtunia mhusika wake mku Zena kuonyesha maonevu ya kijinsia yanayoendezwa katika maswla ya mpigaji kura na uongozi.
- Anatuonyesha jamii ambayo mwanamke anachukuliwa kuwa hawezi kuongoza. Ndiyo sababu hata katika elimu watoto wengi wa kike wananyimwa.
- Kutokana na mwandshi,uzindushi wa kielimu na uongozi aliopata zena kutoka kwa rafiye carol, ulimfanya Zena kuwa mkakamavu kiasi kwao. Hili ni jambo ambalo halijawahi kuonekana katkika jamii hii.
- Anatuchorea jamii iliyojengeka katika tasubi za kiume. Ajabu ni kwammba hali imewaingia hata wanawake wenzake.
- Anaonyesha namna jamii hii ilivyo mbali kuukubali uongozi wa mwanamke.
- Uongozi hutawaliwa na kiasi cha fedha alichonacho mtu. Maskini Zena hangeweza kuwaleta wapiga kura kutoka mabli na kuwalionga wampigie kura.
- Umma usiomjua wajibu wao katika kutena viongozi
- Umma hauoni uwezo wa kwa wa kubadilisha maisha yao bali wako tayri kuuza kura zao.
- Anaonyesha ilivyo vigumu kwa mwanamke kupata nafasi ya uongozi.
- Mwandishi ana matumaini kuwa hali inawez kubadilika kutokana na majuto ya badhi ya wakaazi wanaoonekana kujiuma vidole wakijuta (zozote 10X2) ala. 20
2.
- Zena kunyimwa haki ya kuendelea na masomo
- Zena kuozwa mapema
- Zena kupigwa na Ali.
- Zena kutusiwa [ Iteuzi]
- Kuumia wembe mmoja kuchanjia wateja wengi – ulaghai.
- Uasherati [ siku ya Mganga]
- Bintiye Mavitu kutungwa momba na jirani.
- Mavitu kunya ng’unywa kijishamba na jirani.
- (Kachukwa hatua Nyingine)
- Ulagahi wa salim _ (pwagu)
- Mawaziri kukojoa ndani yam to.
- Hongo na mirungura. [ Mayai Waziri……..]
- Tanbihi:
- Lazima mtahiminwa ataje hoja kasha atambue hadithi. (zozote 10×2) ala. 20
3 Ni kweli kuwa kezilahabu ametumia jazanda nyingi na ndoto katika uandishi wake
i) jazanda/ ndoto
Watoto kumi waliodhoofika afya yao
Wanadhihirisha umaskini na shida hata ya miaka ya uhuru
Katika ile ajali, dereva na mama hawakufa ilhali ukombozi alikufa, dereva anasimamia kiongozi wa nchi na mama ni nchi yenyewe
Kipofu anayepiga ngoma kumi inasimamia viongozi wasiokuwa na mwelekeo au maneno mema kwa taifa
Ile lama ya “X” iliyoandikwa na ukombozi kwenye picha za viongozi wa baraza la mawaziri inaonyesha viongozi hawa ni wabaya, hawajahudumia nchi ipasavyo
Kifo cha ukombozi ni jazanda inayoashiria kuwa wananchi hawakupata ukombozi waliotarajia baada ya uhuru. Waliendelea kuzama katika madhila umaskin na shida
Katika ndoto moja, tunaonyeshwa watoto waliodhoofika na wanapewa chakula na ukombozi wanakula na kukimaliza; ishara ya njaa nchini
Katika ndoto ya pili ukombozi anatumia vitabu vya wenzake kupandia juu ili kufikia picha za mawaziri na kuziwekea alama ya “X” kudhihirisha hawajafanya kazi ya ipasavyo zozote 4×5=20
4. a) Anayesema maneno haya ni likono
Anajisema yeye mwenyewe (tashtiti)
Yuko katika hospitali ya Kenyatta alikopelekwa na mwuguzi Fulani baada ya kugongwa na gari kasha kupelekwa hospitali amabko hangeweza kugharamia malipo ya matibabu
Bwana aliyemgonga alipotelea mbali hakumshughulkia kwa vyovyote zozote 4×1=4
b) Ni kweli hii ni dunia ya dua la kuku halimpati mwewe, maanake wanyonge wananyanyaswa
na kudhulumiwa na matajiri kama ifuatavyo:
– Kizito hakutaka kumpleka likono hospitali licha ya kwamba yeye ndiye aliyekuwa na
makosa alipomgonga
Aidha kizito alidhihirisha madharau kwa kuwaita watu “wajinga wa pira”
Kizito alitoka garini polepole kwa tahadhari asikanyage maji ilhali Likoni alikuwa amelala mle majini.
Kizito hakufurahi Likono alipowekwa katika gari lake kwani aliona angelichafua.Haonyeshi huruma kwa Likoni.
Kizito alimpeleka Likono katika hospitali ya Gipfu na kumwacha huko bila kumlipia gharama ya matibabu.
Dhuluma vilevile inadhihirika pale ambapo daktari Gipfu anataka malipo kabla ya kumhudumia Likono.
Aidha daktari wa Gipfu alipendekeza upasuaji wa Likono ilhali mgonjwa hakuhitaji huduma za aina hiyo.
Dhuluma vilevile inaendelezwa na mwajiri wa Likono anapomwachisha kazi ilhali alielewa
fika kuwa likono alikuwa mgonjwa. zozote (8×2=16 halimpati Mwewe’
5. “Ndimi za mauti” na Arege
(a) Muktadha (al. 4)
(i) Ni sauti akilini mwa Mbunda
(ii) Yeye na wenzake Kamalina na Musesi walichoma bweni ili kumwadhibu mwalimu mkuu.
(iii) Wanafunzi wenzao walichomeka ndani wakiwemo rafiki zao
(iv) Watu walilaani waliotekeleza kitendo hicho
(v) Mbunda aliamua kujisalimisha kwa askari (zozote 4×1=al.4)
(b) Mbinu za uandishi (al. 2)
(i) Ushairi/wmbo
(ii) Takriri
(iii) Sauti (zozote 2×1=al. 2)
(h) Uhalisia katika ‘Ndimi za mauti’ (al. 4)
(i) Malezi mabaya ya watoto
– Mbunda anasema ya kwamba hajawahi kugombezwa na hata kuadhibiwa na babake
(ii) Adhabu ambazo zimepita mipaka/katili /zza kinyama
– Mwalimu mkuu kuwaadhibu wanafunzi na kuwakasirisha hadi kuchukua hatua ya
kuchoma bweni
(iii) Kanuni/sheria za shule ambazo zinawanyima wanafunzi uhuru ;kamaliza anadai kuwa
wao ni mahabusu wa mwalimu mkuu shuleni
(iv) Mapuuza ya wale wenye mamlaka
Tume inaandaliwa kuchunguza uongozi wa mwalimu mkuu baada ya wanafunzi kuchoma bweni na wanafunzi wenzao
Viranja na walinzi kukosa kutambua njama ya wanafunzi kuchoma bweni na kuzuia kutokea kwa tendo hilo
Wazima moto kufika kama wamechelewa shule kukosa vifaa vya kushughulikia mikasa ya dharura kama vile moto shuleni
(v) Majuto kama mjukuu
– Kamaliza na Mbunda kujutia uchomaji shule na kujisalimisha kwa vyombo vya
usalama/ askari
(vi) Uchomaji wa shule kama njia ya kuwaadhibu viongozi wa shule
- Kamaliza anasema kuwa uchomaji wa bweni ni njia ya ‘kumshutua’ mwalimu mkuu kwa kuwaheshimu/kuwakazia.
(vii) Uteuzi wa Tume za kuchunguza majanga na uhalifu baada ya tukio/hasara kutotendeka
- Uchunguzi ulianzishwa kuchunguza uongozi wa mwalimu mkuuu wa shule baada ya bweni kuchomwa
- Askari wanaanza kutafuta aliyehusika katika uchomaji wa bweni baada ya bweni kuchomwa
(viii) Majengo yasiyozingatia viwango vya usalama
- Bweni la wanfunzi lilikuwa limekomelewa kwa nje
Madirisha yalikuwa yamewambwa kwa vyuma /nyaya kwa madai ya usalama wa wanafunzi
6. (II) Umuhimu wa Gege
(a)- Ametumiwa kuonyesha madhara ya tamaa. Tamaa huwafanya watu kutenda maovu.
(Gege anakubali kumuuwa nduguye ili apate mali)
(b)- Ujinga ni kizingiti cha mabadidliko ya kweli katika jamii
(c) – Ukatili haulip chochote. Gege hakufurahia vitu alivyovikamia
II. MKIMBIZI – MWONGOZO
- Vifo – watu wengi walikufa
- Nyumba zilichomwa moto
- Kutengana kifamilia
- Ukosefu wa chakula
- Ukimbizi
- Kusafiri kwa mwendo mrefu- uchovu
- Tisho la kuuwawa
- Masomo kukatizwa
- Mazingira mabaya – kulala kwenye baridi
- ukosefu wa usalama
- Kuathiriwa kisaikolojia – baada ya kuona miili ya waliokufa
- Maradhi/magonjwa ya kuambukizwa
- Uharibifu wa mali
- Uhitaji wa habari kutokana na ukosefu wa vyombo vya mawasiliano
7. a) Muktadha
- Anayezungumza ni (msimulizi) ambaye ni mhusika mkuu/ mkimbizi
- Wako njiani wakitorokea nchi jirani
- Alikuwa na wakimbizi wenzake wakitoroka vita walipotishwa na askari na kuwafanya wasimame ghafla kwa uoga na hofu
- Ni katika hofu hiyo iliyomtia kuyatamka maneno haya kuhusu askari waliokuwa mbele yao
b) Mbinu
- Taswira – jinsi walivyosimama …………….. ardhini
- ii) Tashbihi- kama tumesimikwa
c) Kwa nini akakumbuka mama na ndugu zake
Aliona miili ya wafu (maiti) iliokuwa imetapakaa kila mahali
d) Matatizo ya wakimbizi
- Maradhi k.v. kipindupindu na kifua kikuu
- Uhaba wa hakula
- Vifo njiani k.m. Jesse
- Ukosefu wa usalama wa wakimbizi
- Ukosefu wa maji safi ya matumizi
- Tatizo la kuvuka mto baluke ulipokuwa umefurika
e) Maudhui yanayoibuka:
- Vita – watu kupigana kusababisha ukimbizi
- Ukabila – kati ya walutu na watutsi
- Vifo – kutokana na vita pia magonjwa
- Utengano – familia zilitenhana
- Hofu/ woga – ilioletwa na vita, watu kuuawa
8. (i) MAKULU
Mtu aliye na nafasi. Anampa Nanda kibarua na kumplipa. Ni muhimu kwa kuwa anawasaidia wakazi wa eneo lile pale wanapokuwa hawana hela.
Ni Mkarimu – kuwapa watu bidhaa ili kuwakopesha kama Nanda kuuza mihadarati.
- Anawaajiri watoto wadogo. Mfano ni Nanda ambaye anaajiriwa na kupewa zawadi na pesa.
- Ni mkosa maadili – kule kuwatumia watoto wadogo kulangua mihadarati
- Ni msiri kwa kuwa anayafanya haya yote bila kumwambia yeyote
- Ni mwenye bidii- Aendesha duka kwa bidii. Analima mashamba yake
- Ni mnafiki kwa kuwa anajifanya rafiki mkubwa wa Mzee Atanasi huku akimharibu mwanaye.
- Ni mwongo kwani Mzee Atanasi aliwahi kumweleza kuhusu mabadiliko ya Nanda na akasema yeye hana habari na mabadiliko hayo.
Umuhimu wake:-
- Anatusaidia kufahamu kuwa sio vyote ving’aavyo ni dhahabu
- Ni kielelezo kuwa matajiri wengi hawakutajirika vivi hivi
- Tunajifunza kutowaamini watu wengi hadi kuwapa watoto wetu kuwafanyia kazi
(ii) MWALIMU
- Anaielewa taaluma yake. Anafuatilia maendeleo ya mwanafunzi wake Nanda
- Anawajibika . Ndio sababu amwita babake Nanda ili wajadiliane juu ya mabadiliko ya Nanda
- Ni mshauri mwema. anamshauri Mzee Atanasi la kufanya ili kumwokoa mwanaye
- Anajua kuweka miadi. Alimwalika Atanasi afike mapema naye amesubiri
- Ni mtu makini sana. Ndio sababu ametambua mabadiliko ya Nanda miongoni mwa wanafunzi wengi
Umuhimu wake
- Kielelezo cha umuhimu wa kuwajibika kwa walezi wa kila nui
- Ni kielelezo cha ulezi bora
- Anatuonyesha umuhimu wa kuwa makini kazini
(iii) MZEE ATANASI
- Si makini- mwanaye anaonyesha mabadiliko naye hana habari.
- Ana mapuuza. Yale mabadiliko anayoyaona katika maisha ya Nanda anayapuuza na kuchukulia tu kuwa mtoto anakua
- Ni mshirikina . Akiambiwa kuwa mwanaye kabadilika anachukulia kuwa amerogwa na jirani yake Andanda.
- Ni Mzembe. Amezembea jukumu la kumlea Nanda
Umuhimu wake
- Kielelezo cha wazazi wasiowajibika
- Kielelezo cha hasara inayoweza kutokana na kuamini mambo ya ushirikina
- Ni kielelezo cha urafiki wa chati
- Ni kielelezo cha hasara inayotokana na ukwepaji wa majukumu
(Makulu – al. 7, Mwalimu al. 7 Atanasi – al. 6 = al. 20)
9. (a) (al. 5) – Mkimbizi
- Kukatizwa kwa masomo
- mauaji
- uharibifu wa ali
- uhasma miongoni mwa makabila
- magonjwa/maradhi
- kutamauka(kukata tamaa)
- kugura maeneo
- njaa na kukosa malezi
- kukabilia nahatari (hoja zozote 5x 1= al. 5)
– Fumbo la mwana
Kuzorota kwa masomo
kuzorota kwa afya
kuzorota kwa usafi
uvunjaji wa uhusiano
kutowajibika (zozote 5×1 = al. 5)
(b) Uteuzi wa moyoni
-Kukatizwa kwa masomo kwa wanawake
– Udhalimu dhidi ya wanawake
– Kunyimwa nafasi katika mambo ya siasa
– Chombo cha mapenzi
-Kutukanwa na kuteswa
– Kutokuwa na suti (zozote 5×1=al. 5)
Ngome ya nafasi
- Ndoa ya lazima
- – Kukatizwa kwa masomo
- – Hawana uamuzi
- Hawana sauti
- – Kudhulumiwa
- udhalimu kutoka kw awanawake wengine
- kukandamizwa na sheria (zozote 5×1= al. 5)
10. a)
- Dereva alimgonga Likono kwa gari lake
- Alitaka kutoroka lakini alimlazimisha kumpeleka hospitalini
- Alitaka kuficha ukweli kuwa hakuhusika katika ile ajali ila tu alijitokeza kama mwokozi
b)
- Msamaria mwema halisi (katika biblia) alimpa huduma ya kwanza mgonjwa wake jambo ambalo Dereva hakufanya
- Alimbeba bila kumshurutisha na yeyote
- Aligharamia mahitaji yote jambo ambalo Dereva hakufanya
c) Dereva si mzingatifu
Aliendesha gari huku akiongea katika rununu yake
Barabara mbovu mfano Vidimbwi vya maji machafu
Utovu wa utu na kuthamini sana gari lake – angeweza kumgonga binadamu kwani hana thamani yoyote ukilinganishwa na gari lake ‘Toyota Prado’
Likono pengine alizama katika mawazo sana kuhusu masaibu yaliyomkumba, na ghafla kugongwa Zozote 3×2=6
d)
- Anapoulizwa kilichotendeka, alisitasita dhihirisho la uongo- alipanga atakayosema mfano alijikohoza kikohozi cha bandia kabla ya kusema
- Usamaria wema wake hungefika tu plae yaani kumleta hospitalini bali angemshughikia zaidi
- Dereva na mwenye gari wanatoroka wakidai kwenda kutafuta pesa
- Mwenye gari anafika mwanzo wanaenda chumba ‘Nzengwe’. Wanaongea huku wakitupa macho ya kuibaiba – Ishara ya kupanga watakayosema
- Dereva na mwenye gari wanajaribu kumchanganya Likono kimawazo ati kagongwa na ile “Nissan Prado’ ilihali alijua visuri gari yake ni Toyota Prado Zozote 4×2=8
11. A. Mbinu ya majazi
i) kachukua hatua nyingine – mavitu – mwenye mali /mambo mengi
– Shemeji – mke wa ndugu
ii) Msamaria mwema – Kzito – uwezo/ tajiri
iii) Pwaguzi – Shehe – kiongozi wa dini ya kiislamu
iv) Tuzo – Kibwana – mtu anayejiona mkuu bila ukuu
v) mayai waziri wa maradhi – Ukombozi
– Mayai mtu ovyo
– Dr. Pondamali
B. Mbinu rejeshi
i) kachukua hatua nyingine
– Sakira kukumbu jinsi nduguye alivyomsaidia
– Sakira anakumbuka alivyoacha kazi na kujuta
ii) Fumbo la mwana
iii) Mkimbizi – Anakumbuka walivyouawa wazazi
- Anakumbuka alivyokufa jesee n amzee savalanga
iv) Anakumbuka wosia wa mzee savalanga
12. (a) Uteuzi wa moyoni
- Wanawake wanapigwa na wanaume zao
- Ndoa za lazima
- Kufanyishwa kazi nyingi za nyumbani
- Kupewa elimu duni – darasa la nne, tano
- Kuitwa Malaya
- Kuadhibiwa na waume zao
- Lawama za kutopata watoto ziliwekewa wao
- Kutofaulu kwa ndoa walilaumiwa wao
- Mwanamke anajukumu la kumfurahisha mwanaume
- Kuozwa kwa mabinti mapema
- Mabinti kuachishwa masomo ili waolewe (10×1=10)
(b) Ng’ombe ya nafsi
(i) Mabinti kuozwa mapema
(ii) Kuachishwa shule ili kuolewa
(iii) Kuozwa kwa lazima
(iv) Wanawake kupigwa
(v) Wanawake kuunga mkono utamaduni unaonyanyasa
(vi) Wanawake kutishiwa talaka
(vii) Utamaduni ulikubali ubakaji wa wanawake
(viii) Wanawake kulaumiwa kwa kutopata watoto
(ix) Msichana kutumiwa kuchumia mali
(x) Wanawake kutopewa nafasi ya kuchangia maswala ya ndoa (10×1=10)
13. Masuala Ibuka
i) Ukimwi – siku ya mganga
– Mwaibale anausambaza kwa wembe
– wagonjwa/ wateja wamekondeana na kudhoofika kiafya
ii) Haki za watoto i) Kuchukua hatua nyingine
– watoto kukosa sare, karo, chakula na kwenda shuleni
– Ajira ya watoto
– Mtoto kupachikwa mamba
ii) Fumbo la mwana
– dawa za kulevya
iii) Ngome ya nafsi
– Watoto kuozwa mapema
iv) Uteuzi wa moyoni
– Ndoa za mapema
– wasichana kukosa elimu
iii) Ufisadi – Mayai waziri, waziri fisadi, wizara ya mlungula
– Msamaria mwema – Bw. Kizito Kibambo
– Uteuzi wa moyoni – wapiga kura kuuza kadi zao
– Ngome ya nafasi – Chifu alihongwa, kuficha wahalifu
iv) – Matumizi ya dawa za kulevya/ mihadarati na madhara yake kwa vijana
Fumbo la mwana
Nanda anatumia dawa za kulevya
Anazorota kimasomo, mchafu n.k
v) Ndoa za mapema kwa wasichana
– Zena aliozwa mapea – uteuzi wa moyoni
– Ngome ya nafsi – Naseko anaozwa kwa mzee
vi) Migogoro shuleni
Ndimi za mauti – Wanafunzi kuchoma wenzao bwenini
Mayai waziri – Migomo ya walimu
vii) Vita vya kikabila na suala la wakimbizi
Mkimbizi
ix) Uongozi mbaya – Kuchukua hatua nyingine
Uhalifu wakati wa kura
Viongozi walikosa uwajibikaji
Chifu kuuza chakula kilichotolewa bure wakati wa ukame
Serikali ilifutilia mbali elimu ya bure na kusababisha maskini
Mayai waziri wa maradhi
Waziri mayai
Viongozi walafi
x) Uhalifu katika jamii
– Pwaguzi
– Salim ni tapeli na mizi mkuu
– Kuchukua hatua nyuingine
– Ngome ya nafsi
xi) Umaskini
kuchukua hatua nyingine
fumbo la mwana
msamaria mwema
mayai waziri wa maradhi
xii) Haki za wanawake katika jamii
Uteuzi wa moyoni
Ngome ya nafsi
Kuchukua hatua nyingine
Mayai waziri wa maradhi
Mayai haishi na mkewe
14. Dhamira ni lengo/ nia ya mwandishi wa ‘Tuzo’
i) . Anaashiria kauli kuwa yote yaweza yakatokea hata yasiyotarajiwa k.m. Salome na
kibwana hawana mkabala mzuri lakini Salome anakuja na kumletea habari. Mwandishi
aonyesha kuwa hafla ama matukio huleta wengi pamoja hata wasiosemezana wala
kuamkuana
ii) Anaonyesha kuwa mapeni ni msingi wa mengi. Nia ya kibwana unapokataliwa inakuwa
chanzo cha kutosemezana kwao tena
iii) Anaonyesha kuwa kunao, wakaao pamoja na kufanya kazi pamoja lakini hawana mkabal
mzuri, wao husemezana tu kwa sababu ya kikazi walakini wakitoka nje wanakuwa
mjamba miwili isiyoamba. Salome na kibwana wanasemezana wakati wa kazi
iv) Pia anatuonyesha kuwa kuna wenye vitendo vizuri vyenye sifa. Vitendo vyao vinajulikana
wazi wazi (kama saui zao)lakini wenyewe hawajui vitendo vinaweza kumtambulisha mtu.
v) Kuna haja ya kumtuza aliyefanya vizuri wanahabari wanatuzwa akiwemo Salome Dzoro
vi) Hamu ya kutuzwa huwa hasa katika sherehe ambayo mtuzwa hajatengezwa hadharani.
Tunaiona hamu aliyonayo kibwana
vii) Pia anasisitiza umuhimu wa kauli tahadhari kabla ya athari na kuwa mwangalifu
Anaonyesha umuhimu wa kuwaza kabla ya kutenda
Kibwana angalichunguza kwa makini hangeaibika machoni pake vile.
Tunaelewa alichanganyikiwa hadi katika choo cha wanawake
viii) Anathibitisha ukweli wa methali mzaha
Mzaha hutubga usaha
Mzaha wa Salome wa kumtania kibwana unamletea aibu na kuvurugika akili
ix) Anaonyesha jinsi kutaniana na kuchezeana shere kamwe hakufai. Hii huweza kuleta vita
namna kibwana alitaka walakini akajizuia
x) Anataka kuonyesha jinsi furaha huathiri akili. Kibwana alizidiwa na furaha na kusahau
kuwa anaweza kutaniwa. Mwandishi anaonyesha kuwa kuna kilio au aibu inayoweza
kutokana na futahi hiyo
xi) Anataka kuashiria kuwa vita sio suluhisho kwa kosa ulilotendewa. Kibwana alifumbata
konzi kutaka kuirusha walakini anajizuia. Hili ni funzo dhabiti kuwa haitupasi kusuluhisha
kwa vita
xii) Ni kawaida kuoa anayetuzwa akiringa ama akitembea kwa madaha. Tunaambiwa kuwa
Salome alitembea kwa ndweo kwenda kuitwa zawadi yake. Zozote 10×2=20
15. a) Muktadha
- Msemaji ni Kaloo
- Anamwambia Mwelusi
- Kaloo alikuwa anaanda uwanja kwa mkutano wa kiongozi alipomwona Mwelusi
- Anapomwuliza anachofikiria anajibu kuwa anafikiria misha ya wananchi wote.(Al 4×1=4)
b) Ushahidi wa kudhihirisha kauli hii
- Gege nduguye Mwelusi anapenda kucheza ala ya muziki
- Yuko tayari kumsaliti nduguye kwa ahadi kuwa ataozwa binti wa Bokono Alida
- Muda wake anautumia kuzurura tu na kushiriki katika starehe na anasa
- Yeye hajali wala hashiriki katika shughuli za ukombozi wa Butangi (Zozote 3×2=6)
c) Mchango wa vijana
- Kuwaza kuhusu maisha ya umma
- Wanapigania ukweli na amani – Azena, Mwelusi, Andua
- Wanapinga mateso, Mwelusi
- Wanatetea uhuru, haki na heshima kwa kila mwanabutangi – Mwelusi
- Wanataka kutatua matatizo ya raia
- Wanawafahamisha wananchi kuhusu haja ya utawala wenye msingi wa haki – Mwelusi
- Wanahimiza maendeleo kwa wote
- Wanatumia maarifa kuondoa dhuluma k.m Atega kutumia mkate wa wishwa na tupa
- Wanaasi utawala usiofaa m.f Andua kuteka maji katika kisima cha mkomani
(Alama zozote 10 x1 = 10)